+255 738 785 651
info@cmt.go.tz
Baraza la Masoko ya Mitaji linatoa jukwaa huru na lisilo na upendeleo ili kupitia maamuzi yaliyofanywa na Mamlaka. Huduma hii inahakikisha kuwa hatua za kiusimamizi zinazochukuliwa zinazingatia sheria, zinakuza usawa, uwazi, na uwajibikaji kwenye masoko ya fedha nchini.
Mtu yeyote ambaye hajaridhishwa na uamuzi wa Mamlaka anaweza kukata rufaa kwenye Baraza, akianza na Tangazo la Nia ya Kukata Rufaa ndani ya siku saba (7), likifuatiwa na Maelezo ya Rufaa ndani ya siku thelathini (30) tangu uamuzi ufanyike. Baraza hujiridhisha endapo uamuzi wa mamlaka umezingatia sheria, unaheshimu taratibu za usawa, na unalinda haki za mwekezaji.
Kwa kupitia maamuzi ya kiusimamizi, Baraza linakuwa ulinzi dhidi ya maamuzi holela au yasiyozingatia haki, na hivyo kukuza imani kwenye mfumo wa masoko ya mitaji na kuhakikisha kuwa washiriki wote wanatendewa sawa chini ya sheria.